BREAKING NEWS


Wananchi mkoani Kilimanjaro wamekuwa na taharuki ya ugonjwa wa ebola mkoani hapo baada aliyedaiwa kuwa mgonjwa wa ebola kufikishwa katika kituo cha shirimatunda ambacho kimetengwa na mkoa kwa ajili ya kushughulikia suala hilo.

Na kwa taarifa zilizopo hadi sasa ni mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama amethibitisha kuwa “ni kweli kituo  cha shirimatunda kimetengwa kwaajili ya watu wenye ugonjwa wa ebola kufanyiwa uchunguzi, ila kwa mgonjwa aliyefikishwa hapo amepimwa na kuonekana hana maambukizi ya ugonjwa huo ila alihisiwa na madaktari”

 “alisema Gama”

Hata hivyo mkuu huyo wa mkuu wa mkoa atakutana na waandishi wa habari hii leo majira ya saa nne na imani ni kwamba atazungumzia suala hili.

Endelea kusikiliza redio Boma Hai Fm na kutufuatilia katika mtandao wetu kwa taarifa zaidi.

Na Edwine Lamtey 0758-129 821

No comments:

Post a Comment