Wednesday 19 November 2014
CRDB Bank tunasiliza wateja
kushoto katika picha ni mkurugenzi wa CRDB kanda ya kaskazini ndugu Fransis Moleli na wapili ni meneja wa crdb-Hai ndugu Shirima huku watatu ni meneja wa CRDB-siha bi. Lightness Tarimo wengine ni baadhi ya wafanyakazi wa hospitali hiyo kibong'oto wilayani siha wakati walipokabidhi magoro, vyandarua na sabuni hospitalini hapo.
Picha na Edwine Lamtey
katika picha aliyeshikilia godoro ni mmoja kati ya wauguzi hospitali ya kibong'oto akipokea msaada wa magoro yaliyotolewa na banki ya CRDB-Siha
Picha na Edwine Lamtey 0758-129-821
Tuesday 18 November 2014
CRDB- SIHA YAMWAGA MAGODORO,VYANDARUA NA SABUNI HOSPITALI YA KIBONG'OTO.
Benki ya CRDB inayomjali na kumsikiliza mteja kupitia tawi la Siha lililopo mkoani Kilimanjaro katika wilaya ya Siha imewatembelea wateja wake katika hospitali ya Kibong’oto ambapo wamegawa magodoro,mashuka na sabuni kwa ajili ya watoto na kuahidi kuwa bado itaendelea kutoa misaada mbalimbali ili kujenga mahusiano makubwa zaidi na wateja wao.
Akikabidhi msaada huo mkurugenzi wa benki ya CRDB mkoa Kilimanjaro Fransis Moleli amesema kuwa banki hiyo inatambua umuhimu wa wateja wake hivyo kwa kupitia siku ya wateja duniani(CUSTOMER SERVICE WEEK) imeamua kutoa msaada huo ili kusema Asante kwa wateja wake.
Akipokea msaada huo daktari mkuu katika hospitali ya kibong’oto Dr. Kisonga Riziki amesema kuwa anaishukuru benki ya CRDB kwa msaada walioutoa hii ikiwa ni njia pekee ya kuendelea kuwajali wateja wake pamoja na kushiriki huduma za kijamii na kuzitaka taasisi nyingine kuiga mfano huo.
Kwa upande wake meneja wa CRDB-Siha bi. Lightness Tarimo amesema kuwa katika kupanua huduma za kifedha CRDB ina mfumo wa kufanya miamala mbali mbali kwa njia ya simu iitwayo SIMBANKING hivyo ni vyema wananchi wakatumia fursa hiyo ili kujipatia huduma kwa urahisi.
Pia amewakaribisha wafanyakazi wa hospitali hiyo kujipatia huduma mbalimbali kama vile mikopo,kufungua akaunti n.k
Pia amewakaribisha wafanyakazi wa hospitali hiyo kujipatia huduma mbalimbali kama vile mikopo,kufungua akaunti n.k
Aidha pia Bi. Lightness amesema kuwa msaada ambao umetolewa ni ishara ya kuonyesha kuwa benki itazidi kushirikiana na hospitali hiyo pamoja na vyombo vingine vinavyotoa huduma kwa jamii ili kuimarisha mahusiano mazuri zaidi kwenye utoaji wa huduma bora kwa jamii.
Hospitali ya kibong’oto ni hospitali maalumu ya kutoa huduma kwa magonjwa ya kuambukiza kama vile kifua kikuu na magonjwa mengine.
Na Edwine Lamtey
Thursday 6 November 2014
WAALIMU WAPEWE HAKI ZAO ZA MSINGI.
WITO
umetolewa kwa serikali kuepusha migogoro ya kimaslahi baina ya waalimu na
serikali kuwapa waalimu haki yao ya msingi ya kupata
mshahara kwa wakati.
Hayo
yamesemwa na katibu wa chama cha waalimu wilaya ya hai Samweli
Nyakrere wakati akizungumza na redio Boma Hai Fm ofisini kwake.
Amesema kuwa
kutokana na madai ya muda mrefu kutokea mwaka 2008 kutokupewa kipaumbele katika
kulipwa kwa wakati hali inayochangia kuwepo kwa migogoro baina ya serikali na
waalimu.
Ameongeza
kuwa katika upandishwaji wa madaraja kwa
waalimu bado hawapandishwi madaraja jambo linalo pelekea waalimu kukata tamaa
na kazi yao
huku sera ya serikali ikiwa ni matokeo makubwa sasa.
Kwa upande
wake meneja wa saccos ya waalimu wilaya ya hai bi. Pendo Lyatuma amesema kuwa kutokana na changamoto
mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi wa serikali wameweza kutoa mikopo kwa
riba nafuu kwa wafanyakazi wa serikali na wasio wa serikalini pamoja na kuwapa
mikopo waalimu kusoma na kuongeza elimu yao.
Aidha
Lyatuma ametoa wito kwa wanachama kuona umuhimu wa kuweka akiba katika saccos
wanazo kopa kwaajili ya kuwasaidia kwa maisha ya baadae.
Na Latifa Boto.
MBOWE - HAI LAZIMA IWE SAFI KUANZIA SASA
Mbunge Wa Jimbo
la Hai Mkoani Kilimanjaro Freeman Mbowe
amesikitishwa na kitendo cha mji mdogo wa hai kuendelea kuwa na uchafu, pamoja
na kwamba aliaznisha mpango wa kusafisha mji huo.
Akizungumza
na wananchi katika mkutano wa hadhara ulio fanyika katika mji mdogo wa bomang'ombe amesema kuwa kitendo
cha madiwani kushindwa kutekeleza
mpango wa kufanya usafi kimemsikitisha jambo ambalo limemlazimu kutafuta
mbinu mbadala.
Mbowe
amesema pamoja na viongozi hao kushindwa
kusimamia suala hilo
la usafi ameamua kuweka mikakati thabiti itakayo saidia kuondokana na hali ya
mji kuwa mchafu kwa kutoa vitendea kazi mbalimbali kwaajili ya kufanyai usafi.
Amefafanua
kuwa ili kukabiliana na hali ya uchafu
ametoa gari la kubeba taka lenye tani 30 kwaajili ya kubeba taka katika masoko
mbalimbali ndani ya wilaya ili kunusuru afya za walaji na wafanya biashara
wanaotoa huduma mbalimbali katika masoko yaliyo ndani ya wilaya ya hai kama vile soko la walaji Hai mjini, soko la masama mula, soko la kalali pamoja na masoko mengine.
Akizungumzia
suala zima la huduma ya afya amesema kuwa ili kuondokana na tatitio la gari
maalumu la kubebea wagonjwa (ambulance) ameahidi kutoa gari la wagonjwa kwa hosipitali
teule ya Machame na katika hosipitali ya wilaya ya Hai.
Mh. Mbowe ameongeza
kuwa katika kuhakikisha kuwa njia zina fanyiwa ukarabati wa kiwango kinacho
ridhisha na kufungua njia nyingine kwaajili ya manufaa ya wananchi ametoa
greda itakayo baki ndani ya wilaya siku zote kwa kuchimba na kuchonga
barabara ndani ya wilaya nzima ya Hai ili kurahisisha usafiri.
Aidha pia Mbowe
amewataka wananchi kuchagua viongozi waadilifu na watenda haki katika
uchaguzi wa mwezi ujao desemba wa
uchaguzi wa viongozi wa serikali ya mitaa ili waeweze kutetea haki ya
mtanzania.
Na Devis Minja.
picha na Edwine Lamtey.
Wednesday 5 November 2014
Thursday 23 October 2014
EBOLA YAZUA HOFU KWA WANANCHI MOSHI
Wananchi mkoani Kilimanjaro wamekuwa na
taharuki ya ugonjwa wa ebola mkoani hapo baada aliyedaiwa kuwa mgonjwa wa ebola
kufikishwa katika kituo cha shirimatunda ambacho kimetengwa na mkoa kwa ajili
ya kushughulikia suala hilo .
Na kwa taarifa zilizopo hadi sasa ni mkuu wa
mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama amethibitisha kuwa “ni kweli kituo cha shirimatunda kimetengwa kwaajili ya watu
wenye ugonjwa wa ebola kufanyiwa uchunguzi, ila kwa mgonjwa aliyefikishwa hapo
amepimwa na kuonekana hana maambukizi ya ugonjwa huo ila alihisiwa na madaktari”
“alisema
Gama”
Hata hivyo mkuu huyo wa mkuu wa mkoa atakutana
na waandishi wa habari hii leo majira ya saa nne na imani ni kwamba
atazungumzia suala hili.
Endelea
kusikiliza redio Boma Hai Fm na kutufuatilia katika mtandao wetu kwa taarifa
zaidi.
Na
Edwine Lamtey 0758-129 821
Subscribe to:
Posts (Atom)