Friday 6 March 2015

BRN MAFANIKIO ZAIDI









Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Anne Kilango Malecela akiwa katika picha ya pamoja kati ya waalimu na  wakufunzi  katika semina ya ufunguzi wa matokeo makubwa sasa (BRN)  wilayani Same

Picha Na,
James Gasind 



Naibu Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi Mh Ane Kilango Malecela amewataka waalimu wa shule za msingi waliyo pewa mafunzo ya mbinu bora ya ufundishaji kutumia elimu hiyo ili kunyanyua elimu hapa nchini.

Aliyasema hayo wiki hii wilayani Same alipokuwa katika ufunguzi wa mpango  wa uboreshaji  wa utekelezaji wa matokeo makubwa sasa BRN  ambapo umekutanisha  Wilaya Tano ambazo hazikuweza kufanya vizuri katika matokeo ya darasa la saba mwaka 2012.

Malechela alizitaja halmashauri zilizo husika kupokea mafunzo hayo bora ya ufundishaji ambazo hazikufanya vizuri kuwa ni Rombo,Same,Moshi vijijini,Handeni na Korogwe.

Aliongeza kuwa elimu na mafunzo waliyo pata itasaidia kuboresha elimu katika shule za msingi kwani uwepo wa vitendea kazi pamoja na majengo kuwapo pasipo kuwa na waalimu wanao pewa mafunzo mara kwa mara hakutaweza saidia kuinua elimu hapa nchini ndio maana utekelezaji wa matokeo makubwa sasa umeanza kwa kuwapa waalimu mafunzo na mbinu mpya za ufundishaji.

“Ndugu Waalimu tukisema kuwa tulete vitabu pamoja na miundo mbinu mizuri kuwekwa shuleni pasipo Waalimu kupewa mafunzo mara kwa mara ya mbinu na namna ya ufundishaji ili kukuza taaluma na kuongeza ufauli wa Wanafunzi hapa Nchini bado tutakuwa hatuja piga hatua katika sekta ya Elimu”Alise Malechela.

Alisema kuwa takribaniWilaya 40 zitapokea mafunzo hayo lengo likiwa ni kuwapa waalimu wa masomo ya Hisabati,Kiswahili na Kiingereza mbinu mbadala za kufundisha wanafunzi na kuwagundua mapema wanafunzi ambao wanahitaji msaada zaidi katika kupewa elimu ili kuwe na uwiano mzuri darasani.

Kwa upande wake Mratibu wa mafunzo hayo Lawrence Mwinuka aliipongeza serikali katika kutekeleza sera ya Matokeo makubwa sasa ambapo amewataka waalimu waliyo pokea mafunzo hayo kufanyia kazi pamoja na kuwafundisha waalimu wengine hatimaye kujenga kizazi chenye matumaini katika elimu ya uhakika.

“Tunashukuru kwa kukumbukwa hasa waalimu hawa wa masomo ya Hesabu,Kiingereza na Kiswahili ambapo ni masomo ambayo kwa namana nyingine yanawapa shida Wanafunzi wa shule za Msingi kilichopo ni sisi Waalimu kufanyia kazi mafunzo haya ili kuleta ushindani  wa ufaulu kwa Shule zetu”Alisema Mwinuka.

Naye Mkuu wa kitengo cha habari toka Mamlaka ya Elimu Tanzania Sylivia Lupembe alisema kuwa mpango  uliopo ni kuhakikisha elimu hapa nchini inathaminiwa na kukua kwa kasi ili kuzalisha wataalamu wa fani mbalimbali.

Ilikuhakikisha sera ya matokeo makubwa sasa  BRN inafanikiwa kama ilivyo kusudiwa kwa kiwango kikubwa Malaka ya Elimu Tanzania imetoa wakufunzi 18 toka wizara ya elimu watakao zunguka nchi nzima kutoa elimu kwa halmashauri 40 ambazo hazikufanya vizuri katika matokeo ya darasa la saba 2012 ambapo kiasi cha shilingi milioni 137 zitatumika katika kutoa elimu kwa mafunzo hayo.

Habari Na 
Davis Minja 0769-432367


No comments:

Post a Comment